Thursday, 8 January 2015
Tuesday, 6 January 2015
NAMNA YA KUMSIFU NA KUMWABUDU MUNGU IPASAVYO
Moja ya sababu ya watu kutomsifu na kumwabudu Mungu ipasavyo, ni
kutokujua namna ya kufanya sifa na kuabudu. Mambo/Pointi zifuatazo zitakusaidia
kukuwezesha kujua namna ya kumsifu, kumwabudu na kumshukuru Mungu. Unapokuwa
umetenga muda wa kusifu na kuabudu, au unapokuwa katika muda wako wa maombi,
tumia ufahamu wako juu ya mambo uliyojifunza kuhusu Mungu, yanayomstahilisha kusfiwa
na kuabudiwa. Kwa mfano:-
A: MSIFU MUNGU KWA YALE MAMBO YANAYOMSTAHILISHA
1)
Mtukuze Mungu kwa Sifa zake za kipekee ( Sifa zake za Ki-Mungu).
Mweleze jinsi alivyo Mtakatifu , Wa
milele, Mwenye nguvu zote, Mwenye akili na ufahamu wote, n.k
2)
Mtukuze Mungu kwa Tabia zake.
Mweleze jinsi alivyo mwenye Upendo mwingi usiopimika,
jinsi alivyo na huruma nyingi, jinsi alivyo mwaminifu na wa kweli. Msimulie
habari ulizozisikia na ulizozisoma juu ya tabia zake kwetu.
3)
Mtukuze Mungu kwa Matendo yake makuu.
Mweleze jinsi unavyohusudu
kazi mbalimbali za mikono yake, uumbaji wake, na matendo yake makuu. Msimulie
jinsi unavyokubali ubora wa kazi zake na ukuu wa matendo yake. Msimulie
unavyothamini matendo yake makuu kutoka katika biblia au katika shuhuda
ulizozisikia katika maisha ya sasa ya kila siku.
4)
Mtukuze Mungu kwa Baraka na Fadhili zake.
Msifu na kumshukuru kwa
fadhili na baraka mbalimbali ulizopata kutoka kwake. Kwa zawadi ya uhai, afya
njema, uponyaji, ulinzi, chakula, kazi, elimu, fedha, mali, mifugo, mashamba,
biashara, n.k. Yako mambo mengi sana, Mungu amekutendea, usiyoweza kumaliza
kuelezea. Msifu kwa hayo.
5)
Mtukuze Mungu kwa Ahadi zake nzuri kwetu.
Pia unaweza kumsifu Mungu kwa ahadi zake mbalimbali
alizotupa. Ukampamba kwa jinsi alivyokusudia kutubariki, kutuinua, kutulinda,
kutushindia, kututetea, kutuwezesha, kutusaidia, n.k.
B: MSIFU
MUNGU KWA MAJINA YAKE.
Majina ya Mungu, hueleza sifa
za Mungu, Tabia za Mungu au Matendo ya Mungu. Mfano; Wayahudi wanamwita Mungu El-Shaddai.
Ni neno lenye majina mawili ndani yake. ‘El’ maana yake Mungu, na ‘Shaddai’ lenye maana itokanayo na
neno ‘Shad’
yaani Titi (Ziwa) la mama
anyonyeshaye.
Kutokana na ukweli kwamba,
titi/ziwa la mama anyonyeshaye, linampa mtoto mchanga kila kitu anchohitaji. Maziwa
ya mama yake, humpa mtoto kila kitu mtoto anachohitaji. Ndani ya maziwa kuna
vitamini, protini, wanga, mafuta, madini, maji, na kila kitu mtoto
anachohitaji. Maziwa ya mama, yanamtosheleza mtoto kwa kila kitu. Hivyo,
Waisraeli wanapomwita Mungu El-Shaddai, wanamaanisha kuwa, kama
ziwa linavyo mtosheleza mtoto, vivyo
hivyo, Mungu ni ‘Mtoshelezi’
kwetu. Halleluyah!
Hivyo, kila jina la Mungu,
linabeba aidha Sifa yake au Tabia yake au Matendo yake. Ndio maana Mfalme Daudi
anasema “… Mpeni Bwana, enyi wana wa
Mungu … Mpeni Bwana utukufu kwa jina lake. Mwabuduni Bwana kwa uzuri
wa utakatifu.” (Zab 29:1-2) Msifuni Bwana kwakuwa Bwana ni mwema, Liimbieni Jina lake, kwakuwa
lapendeza.(Zab 135:3). Unaweza kumsifu Bwana kwa
majina yake. Yafuatayo ni baadhi ya majina ya Mungu kwa lugha ya Kiebrania,
yatakayokusaidia kumsifu, kumwabudu na kumshukuru Mungu.
-
TANZANIA BEI YA MAFUTA YASHUKA, EWURA YATAJA BEI MPYA
Mamlaka ya udhibiti wa nishati,maji na mafuta(ewura) imetangaza kushusha kwa bei za mafuta kuanzia kesho (januari 07/2015) kwa nchi nzima. Akizungumza na wanahabari leo ofsini kwake, mkurugenzimkuu wa mamlaka ya Udhibiti wa nishati,maji na mafuta, bwana Felix Ngamlagosi, jijini Daresalaam,
Sasa amevitaja viwango hivyo vipya vya bei za mafta kuwa vitaanza kutumika rasm kesho;-
Bei ya petrol,
Bei ya petrol kwa lita moja itauzwa kwa tsh,1955 hii nikutokana na kushuka kwa asilimia 6 kwa sawa na tsh 311 upungufu iliyo pungua kutoka kwa bei ya awali.
Bei ya Dizeli
Pia lita moja ya dizeli itauzwa kwa Tsh,1845 amabapo asilimia zilizo shuka ni 13 sawa na tsh244 zilizopungua kutoka bei ya awali.
Bei ya mafuta ya taa,
Mwisho mafuta ya taa nayo yatauzwa kwa tsh1833 lita moja.
Baada ya kuvita viwango hivyo vya bei mpya bw Ngamlagosi amewataka watanzania kujenga utamaduni wa kuomba au kudai risiti ya malipo mara tu wanapo nunua mafuta kila wakati..
Sasa amevitaja viwango hivyo vipya vya bei za mafta kuwa vitaanza kutumika rasm kesho;-
Bei ya petrol,
Bei ya petrol kwa lita moja itauzwa kwa tsh,1955 hii nikutokana na kushuka kwa asilimia 6 kwa sawa na tsh 311 upungufu iliyo pungua kutoka kwa bei ya awali.
Bei ya Dizeli
Pia lita moja ya dizeli itauzwa kwa Tsh,1845 amabapo asilimia zilizo shuka ni 13 sawa na tsh244 zilizopungua kutoka bei ya awali.
Bei ya mafuta ya taa,
Mwisho mafuta ya taa nayo yatauzwa kwa tsh1833 lita moja.
Baada ya kuvita viwango hivyo vya bei mpya bw Ngamlagosi amewataka watanzania kujenga utamaduni wa kuomba au kudai risiti ya malipo mara tu wanapo nunua mafuta kila wakati..
| Mkurugenzi mkuu wa EWURA Bw, Felix Ngamlagosi (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari ofsini kwake alipokua akitaja na kutoa maelezo juu ya kushuka kwa bei ya mafuta hapa nchini. |
Monday, 5 January 2015
RAISI KIKWETE AMWAPISHA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI
![]() |
| Raisi Dr Jakaya Kikwete akimwapisha mwanasheria mkuu wa selikali George Mcheche katika ikulu ya Raisi ambapo ndipo hafla fupi ya kumpongeza ilifanyika. |
Ikiwa ni muda mfupi kupita tangu aliye kuwa mwanasheria mkuu wa serikali jaji Fredrick Werema ajiudhulu kufuatia sakata la upotevu wa zaidi ya bilioni miatatu kutoka kwenye akaunti ya tegeta Escrow sasa Raisi wa jamhuli ya muugano wa Tanzania Dr Jakaya Mlisho Kikwete amemteua Mwanasheria mwingine atakaye vaa kiatu cha Werema.
Raisi Kikwete amemteua Georg Mcheche kuwa mwanashelia mkuu wa Tanzania.
![]() |
| Raisi Dr Jakaya Kikwete akisaini mara baada ya kumwapisha mwanasheria mkuu Tanzania George Mcheche ikulu. |
Sunday, 4 January 2015
NDANI YA YESU HAKUNA MZEE BI MAGRET AENDELEA KUMTUMIKIA MUNGU KWENYE HUDUMA YA UIMBAJI
Huu ndio msemo unaweza kuutumia kuwa ndani ya Yesu hakuna mzee hii ni baba ya bi Magreti wa kanisa la fpct tegeta kuonyesha uwezo mkubwa akiwa madhabauni anamwimbia Bwana wa majeshi sauti yake husikika kama kijana lakini kumbe umri umesogea hii imekuwa baraka kubwa katika kanisa la fpct kwani watu wengi ndani ya kanisa hilo wamekuwa wakipata darasa kwa bibi hasa waimbaji inatia moyo sana
bi magreti akiongoza nyimbo za wokovu
bi magreti akiongoza nyimbo za wokovu
Friday, 2 January 2015
HIVI NDIVYO MJI WA MOROGORO ULIVYO PATA SURUBA YA MVUA
![]() |
| Sehem ya soko la Morogoro ilivyo jaa maji huku wakazi wa mji huo na wafanya biashara wakitaabika . |
ya biashara wa soko la Mjini Morogoro walipata taabu na kushindwa kufanya biashara kabisa kwenye soko hilo kufuatia mvuakubwa zilizo nyesha na kupelekujaa kwa mto Kikundi kupoteza uelekeo wa kutiririsha maji na kisha kuya tiririsha maji yake katika mji wa Morogoro..
Thursday, 1 January 2015
ASANTE YESU KWA KUTUVUSHA SALAMA SASA TUMEUPOKEA MWAKA 2015.
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
| Mchungaji NTASEHA (Kulia) akiwa na mzee kiongozi FESTO KIMALI |
Subscribe to:
Posts (Atom)



















