Thursday, 8 January 2015

HII SI YA KUKOSA NI JUMAPILI YA KIPEKEE NJOO UKUTANE NA MJIBU YAKO

NJOONI TUMSIFU NA KULITUKUZA JINA LAKE MAANA YEYE NDIYE ALIYEZIUMBA MBINGU NA NCHI ....NJOO UPATE MSINGI IMARA KATIKA SIKU MUHIMU ....LAZIMA MUNGU ATAZUNGUMZA NA WEWE HAKIKA HII SI YA KUKOSA WAPENDWA

Tuesday, 6 January 2015

NAMNA YA KUMSIFU NA KUMWABUDU MUNGU IPASAVYO



Moja ya sababu ya watu kutomsifu na kumwabudu Mungu ipasavyo, ni kutokujua namna ya kufanya sifa na kuabudu. Mambo/Pointi zifuatazo zitakusaidia kukuwezesha kujua namna ya kumsifu, kumwabudu na kumshukuru Mungu. Unapokuwa umetenga muda wa kusifu na kuabudu, au unapokuwa katika muda wako wa maombi, tumia ufahamu wako juu ya mambo uliyojifunza kuhusu Mungu, yanayomstahilisha kusfiwa na kuabudiwa. Kwa mfano:-


                                A: MSIFU MUNGU KWA YALE MAMBO YANAYOMSTAHILISHA
1)      Mtukuze Mungu kwa Sifa zake za kipekee ( Sifa zake za Ki-Mungu).
Mweleze jinsi alivyo Mtakatifu, Wa milele, Mwenye nguvu zote, Mwenye akili na ufahamu wote, n.k

2)      Mtukuze Mungu kwa Tabia zake.
Mweleze jinsi alivyo mwenye Upendo mwingi usiopimika, jinsi alivyo na huruma nyingi, jinsi alivyo mwaminifu na wa kweli. Msimulie habari ulizozisikia na ulizozisoma juu ya tabia zake kwetu.

3)      Mtukuze Mungu kwa Matendo yake makuu.
Mweleze jinsi unavyohusudu kazi mbalimbali za mikono yake, uumbaji wake, na matendo yake makuu. Msimulie jinsi unavyokubali ubora wa kazi zake na ukuu wa matendo yake. Msimulie unavyothamini matendo yake makuu kutoka katika biblia au katika shuhuda ulizozisikia katika maisha ya sasa ya kila siku.

4)      Mtukuze Mungu kwa Baraka na Fadhili zake.
Msifu na kumshukuru kwa fadhili na baraka mbalimbali ulizopata kutoka kwake. Kwa zawadi ya uhai, afya njema, uponyaji, ulinzi, chakula, kazi, elimu, fedha, mali, mifugo, mashamba, biashara, n.k. Yako mambo mengi sana, Mungu amekutendea, usiyoweza kumaliza kuelezea. Msifu kwa hayo.
5)      Mtukuze Mungu kwa Ahadi zake nzuri kwetu.
Pia unaweza kumsifu Mungu kwa ahadi zake mbalimbali alizotupa. Ukampamba kwa jinsi alivyokusudia kutubariki, kutuinua, kutulinda, kutushindia, kututetea, kutuwezesha, kutusaidia, n.k.

                                   B:                    MSIFU MUNGU KWA MAJINA YAKE.
Majina ya Mungu, hueleza sifa za Mungu, Tabia za Mungu au Matendo ya Mungu. Mfano; Wayahudi wanamwita Mungu El-Shaddai. Ni neno lenye majina mawili ndani yake. El’  maana yake Mungu, na ‘Shaddai’ lenye maana itokanayo na neno ‘Shad’ yaani Titi (Ziwa) la mama anyonyeshaye.

Kutokana na ukweli kwamba, titi/ziwa la mama anyonyeshaye, linampa mtoto mchanga kila kitu anchohitaji. Maziwa ya mama yake, humpa mtoto kila kitu mtoto anachohitaji. Ndani ya maziwa kuna vitamini, protini, wanga, mafuta, madini, maji, na kila kitu mtoto anachohitaji. Maziwa ya mama, yanamtosheleza mtoto kwa kila kitu. Hivyo, Waisraeli wanapomwita Mungu El-Shaddai, wanamaanisha kuwa, kama ziwa linavyo mtosheleza mtoto, vivyo hivyo, Mungu ni ‘Mtoshelezi’ kwetu. Halleluyah!

Hivyo, kila jina la Mungu, linabeba aidha Sifa yake au Tabia yake au Matendo yake. Ndio maana Mfalme Daudi anasema “… Mpeni Bwana, enyi wana wa Mungu … Mpeni Bwana utukufu kwa jina lake. Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu.” (Zab 29:1-2) Msifuni Bwana kwakuwa Bwana ni mwema, Liimbieni Jina lake, kwakuwa lapendeza.(Zab 135:3). Unaweza kumsifu Bwana kwa majina yake. Yafuatayo ni baadhi ya majina ya Mungu kwa lugha ya Kiebrania, yatakayokusaidia kumsifu, kumwabudu na kumshukuru Mungu.


                                                                  

                                  -         

TANZANIA BEI YA MAFUTA YASHUKA, EWURA YATAJA BEI MPYA

Mamlaka ya udhibiti wa nishati,maji na mafuta(ewura) imetangaza kushusha kwa bei za mafuta kuanzia kesho (januari 07/2015) kwa nchi nzima. Akizungumza na wanahabari leo ofsini kwake, mkurugenzimkuu  wa mamlaka ya Udhibiti wa nishati,maji na mafuta, bwana Felix Ngamlagosi, jijini Daresalaam,
Sasa amevitaja viwango hivyo vipya vya bei za mafta  kuwa  vitaanza kutumika rasm kesho;-

Bei ya petrol,
      Bei ya petrol kwa lita moja itauzwa kwa tsh,1955 hii nikutokana na kushuka kwa asilimia 6 kwa sawa na tsh 311 upungufu iliyo pungua kutoka kwa bei ya awali.

Bei ya Dizeli
   Pia lita moja ya dizeli itauzwa kwa Tsh,1845 amabapo asilimia zilizo shuka ni 13 sawa na tsh244 zilizopungua kutoka bei ya awali.

Bei ya mafuta ya taa,
 Mwisho mafuta ya taa nayo yatauzwa kwa tsh1833 lita moja.

Baada ya kuvita viwango hivyo vya bei mpya bw Ngamlagosi amewataka watanzania kujenga utamaduni wa kuomba au kudai risiti ya malipo mara tu wanapo nunua mafuta kila wakati..
Mkurugenzi mkuu wa EWURA Bw, Felix  Ngamlagosi (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari ofsini kwake alipokua akitaja na kutoa maelezo juu ya kushuka kwa  bei ya mafuta hapa nchini.

Monday, 5 January 2015

RAISI KIKWETE AMWAPISHA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI

Raisi Dr Jakaya Kikwete akimwapisha mwanasheria mkuu wa selikali George Mcheche katika ikulu ya Raisi ambapo ndipo hafla fupi ya kumpongeza ilifanyika.

Ikiwa ni muda mfupi kupita tangu aliye kuwa mwanasheria mkuu wa serikali jaji Fredrick Werema ajiudhulu kufuatia sakata la upotevu wa zaidi ya bilioni miatatu kutoka kwenye akaunti ya tegeta Escrow sasa Raisi wa jamhuli ya muugano wa Tanzania Dr Jakaya Mlisho Kikwete amemteua Mwanasheria mwingine atakaye vaa kiatu cha Werema.
      Raisi Kikwete amemteua Georg Mcheche kuwa mwanashelia mkuu wa Tanzania.
Raisi Dr Jakaya Kikwete akisaini mara baada ya kumwapisha mwanasheria mkuu Tanzania  George Mcheche ikulu.
  

Sunday, 4 January 2015

NDANI YA YESU HAKUNA MZEE BI MAGRET AENDELEA KUMTUMIKIA MUNGU KWENYE HUDUMA YA UIMBAJI

Huu ndio msemo unaweza kuutumia kuwa ndani ya Yesu hakuna mzee hii ni baba ya bi Magreti wa kanisa la fpct tegeta kuonyesha uwezo mkubwa akiwa madhabauni anamwimbia Bwana wa majeshi sauti yake husikika kama kijana lakini kumbe umri umesogea hii imekuwa baraka kubwa katika kanisa la fpct kwani watu wengi ndani ya kanisa hilo wamekuwa wakipata darasa kwa bibi hasa waimbaji inatia moyo sana
                                                   bi magreti akiongoza nyimbo za wokovu





Friday, 2 January 2015

HIVI NDIVYO MJI WA MOROGORO ULIVYO PATA SURUBA YA MVUA

Sehem ya soko la Morogoro ilivyo jaa maji huku wakazi wa mji huo na wafanya biashara wakitaabika . 

Kufuatia mvua zinazo endelea nchini hivi ndivyo wafan
ya biashara wa soko la Mjini Morogoro walipata taabu na kushindwa kufanya biashara kabisa kwenye soko hilo kufuatia mvuakubwa zilizo nyesha na kupelekujaa kwa mto Kikundi kupoteza uelekeo wa kutiririsha maji na kisha kuya tiririsha maji yake katika mji wa Morogoro..